Unajua waajiri wanapenda kuona nini kwenye CV yako? Leo tunakuletea vidokezo muhimu vya kuandika CV...Read more
Jinsi Ya kujibu Swali La Mshahara Kwenye Job Interview
- By Admin
- 17 - April - 2024
TUKUBALIANE!
Siku zote interview yako itaenda vizuri, hadi pale linapotokea swali la "UNATAKA KULIPWA TSHILINGI NGAPI?
Ghafla maneno yanakwama, ni kama kitendawili kigumu, kikiacha hata wenye uzoefu kwenye sintofahamu
Jinsi ya kujibu swali la matarajio ya mshahara kwenye Job Interview.
1. Muda ni kila kitu!
Jitahidi kuchelewesha kujadili mshahara hadi upate uelewa wa mahitaji ya kazi na matarajio ya kampuni:
Onyesha nia kujifunza zaidi kabla ya kuamua kuhusu kutaja matarajio yako ya mshahara.
Hata kama kipaumbele chako ni pesa, usiionyeshe moja kwa moja.
2. Elewa Soko:
Kabla ya kuingia kwenye mahojiano, TAFITI, TAFITI, na TAFITI zaidi.
Tumia Nguvu ya Maandalizi ku jijengee data imara kuunga mkono matarajio ya mshahara yenye ushindani na yanayofaa.
3. Weka Wigo (Range) Badala ya Kiasi:
Hakikisha wigo unalingana na utafiti wako wa soko.
"Ningependa kulipwa kuanzia Tsh 600,000 - 850,000"
4. Zingatia Faida Zisizo za Fedha:
Kumbuka, mshahara ni kisehemu kidogo cha fidia.
Usisahau kujadili faida nyingine muhimu kama vile
- Bima ya afya
- Saa za kazi
- Likizo
- Chaguzi za kufanya kazi kwa mbali n.k
5. Jikite katika Thamani:
Weka mkazo kwenye thamani kubwa unayotoa. Onyesha vipaji vyako vya pekee, mafanikio, na jinsi kuwekeza kwako kutakuza mafanikio yao!
Ongelea
- Uzoefu wako
- Mafanikio yanayolingana na majukumu ya kazi.
- Ujuzi wako mwingine
6 Usiwe mkali, kuwa flexible:
Mshahara ni maelewano! Onyesha utayari wako wa kuelewana.
Weka msisitizo kuwa uko tayari kujadili kufanya majadiliano cha mshahara, ikiwa ni pamoja na faida, bonasi, bima, na mafao mengine.
7. Epuka Kufichua Mishahara ya Zamani:
Shh, ni siri????!
Epuka kufichua mshahara wako wa zamani ili kudumisha ushawishi wako kwenye majadiliano.
Fursa hii mpya inaweza kuwa na hadhi na thamani tofauti kabisa.
8. Jiandae mapema:
Jiandae na ujifunze majibu yako kwa swali la matarajio ya mshahara mapema.
Jifanye kama unajibizana na rafiki au jamaa ili upate ujasiri katika kutoa majibu yako kwa urahisi na ufanisi bila kutetemeka.
9. Kuwa mtulivu na mwenye ujasiri
Kujibu maswali ya matarajio ya mshahara kunaweza kuleta wasiwasi, lakini endelea kuwa na utulivu na ujasiri.
Epuka kutoa hisia za kukata tamaa kwa kazi.
10. Kumbuka Ni Mchakato:
Kujadiliana mshahara ni sehemu ya kawaida ya mchakato wa mahojiano ya kazi.
Mwajiri anatarajia mkubaliane kabla ya kuendelea mbele.
Tazama mazungumzo kwa mtazamo wa ushirikiano, ukiwa na lengo la kupata suluhisho la pamoja